Msanii wa bongo fleva Belle 9 mwenye 'hit song' ya 'Ma Ole'
alioshirikiana na G Nako amefunguka kwa kusema hawezi kufanya 'promo' ya
kutangaza muziki wake kwa kupiga picha zitakazo kuwa zinamuonesha mwili
wake kama alivyofanya Ben Pol hivi karibuni.
Belle amebainisha hayo kupitia kipindi cha FNL kinachorushwa na EATV
kila siku ya Ijumaa kuanzia saa tatu kamili usiku mpaka saa tano za
usiku.
"Kwa maadili ya kiafrika na kwa jinsi ambavyo tumezoea sio kitu cha
kawaida ninaweza sema lakini sijui labda anaweza akaja kutengeneza
sababu ambazo zitaendana na zile picha...Kiukweli mimi siwezi, Siamini
katika hilo kuwa muziki wa Ben Pol umeshindwa na upepo ila naona kama
ameenda 'speed' kidogo...Ben Pol ana ujasiri mkubwa " alisema Belle 9.
Subscribe by Email
Follow Updates Articles from This Blog via Email

No Comments