.
Mizizi: Mizizi ya kabichi hutawanyika ardhini vizuri. Kwa kawaida,
huenda chini kiasi cha sentimita ishirini (20 sm), na hujitawanya kwa kiasi cha
sentimita sabini na tano (75sm).
Shina: Shina la mmea wa kabichi huwa na rangi ya kijani au
zambarau. Hii hutegemeana na aina ya kabichi, na kwa kawaida ni fupi.
Aina za kabichi
Kuna aina nyingi za
kabichi na zifuatazo ni miongoni mwa aina hizo:
1. Prize drumhead;Aina hii hukomaa katika kipindi cha miezi 3.5
2. F1-High Breed;Aina hii hukomaa katika kipindi cha miezi 2-4
3. Duncan;Aina hii hukomaa katika kipindi cha miezi 3
4. Early Jersey wakefieldAina hii hukomaa katika kipindi cha miezi 3.5
5. Sugar loaf;Aina hii hukomaa mapema sana, kiasi cha miezi 2.5
6. Glory of enkhuizen;Aina hii hukomaa katika kipindi cha miezi 3.5
Hali ya hewa ifaayo
Kabichi hustawi vyema
katika sehemu yenye hali ya baridi, hali ya joto jingi haifai kwa kabichi kwa
kuwa huathiri uotaji na ukuaji wake. Joto jingi pia husababisha kulegea kwa
vichwa vilivyofunga. Zao hili hustawi vema katika maeneo yenye mwinuko wa zaidi
ya mita 100 toka usawa wa bahari.
Udongo
Zao hili linaweza
kustawishwa kwenye udongo wa aina yoyote mradi tu udongo huo usiwe na
chumvichumvi nyingi na usiotuhamisha maji. Udongo wa kichanga na ule usio na
rutuba ya kutosha husababisha kabichi kukomaa upesi na kuzaa kabichi hafifu
zenye vichwa vidogo.
Kitalu cha kabichi
Kitalu ni muhimu katika
uzalishji wa zao hili. Ni vema kutengeneza matuta yenye upana wa mita moja, na
urefu wowote kulingana na matakwa ya mkulima. Mbolea za samadi na zenye asili
ya chokaa zichanganywe vizuri kwenye udongo. Kiasi cha gramu 500 za mbegu
huhitajika kwa hekta moja. Katika upandaji kwenye kitalu ni vizuri kutengeneza
mistari katika tuta, umbali toka mstari hadi mstari uwe sentimita ishirini
(20). Udongo kiasi kidogo utumike katika kufunika mbegu.
Baada ya mbegu kuota ni vizuri kupunguza baadhi ya miche na uwe katika kipimo
cha sentimita 2-3 toka mche hadi mche. Hii itasaidia kuwa na miche mifupi na
yenye nguvu. Inafaa kunyeshea kitalu mara moja au mbili kwa siku na katika
sehemu za joto ni vizuri kuweka kivuli katika matuta. Katika wiki ya tatu, hadi
wiki ya nne, ni vyema kuondoa kivuli kidogo kidogo huku ukipunguza unyeshaji.
Hali hii itasaidia miche isipate mshtuko wa uhamishaji shambani.
Kuhamisha na kupanda
Hamisha na kupandikiza
miche shambani ikiwa na umri wa wiki nne, wakati huo miche ikiwa na majani
manne ya mwanzoni na urefu wa kiasi cha sentimita kumi na mbili (12). Wakati wa
upandaji, ni vizuri udongo ukashindiliwa kwenye kila mche. Inafaa upandaji
ufanyike mara moja, na ni vizuri ukafanyika nyakati za jioni au asubuhi sana,
na udongo uwe na unyevu wakati wote.
Nafasi kati ya mmea
Katika mstari hadi mstari
inatakiwa iwe sentimita 60-75. Kutoka mmea hadi mmea ni sentimita 30-60. Pia
sentimita 75-90 inaweza kutumika kati ya mstari na mstari.
Mbolea
Ni vizuri kuweka kiasi
cha viganja 2-3 vya mbolea ya samadi iliyooza vizuri katika kila shimo.
Palizi
Wakati wa palizi ni
vizuri mkulima akawa mwangalifu ili asiharibu mizizi. Wakati kabichi inapoanza
kufunga hufunika ardhi, hivyo, husaidia kuzuia magugu yasiote, kwa wakati huu
hakuna haja ya kupalilia.
Kuvuna:
Kabichi hukomaa katika
kipindi cha siku 60-100 tangu kupandwa. Kwa ajili ya kuuza ni vizuri kuvuna
wakati vichwa vinapofunga vizuri na huwa na uzito wa kutosha kabichi iangaliwe
na kutunzwa baada ya kuvunwa ili isikwaruzwe na kuoza kabla ya kutumiwa. Kwa
kawaida hekta moja hutoa mavuno kiasi cha tani 50-80.
Subscribe by Email
Follow Updates Articles from This Blog via Email
No Comments