Utayarishwaji
wa shamba.
Kuandaa shamba kwa ajili ya kulima Tangawizi unaweza kutumia trecta, jembe la
mkono au la ng’ombe kutayarisha shamba, shamba litayarishwe mwezi mmoja kabla
ya kupandikiza kwa kukatua ardhi hadi kufikia kina cha sentimita 30. Lainisha
udongo.
Shamba
linatakiwa kuandaliwa vituta vidogo vidogo kwa nafasi ya sentimita 75 kutoka
tuta hadi tuta, hiihusaidia kuhifadhi udongo na maji na hutoa nafasi nzuri
wakati wa upanukaji wa viazi. Inashauriwa pia kama matuta hayajatumika basi ni
muhimu kujaza udongo kwenye shina kwani pingili za chini kwenye shina ni lazima
zifunikwe na udongo ili zitoe viazi kwa wingi na hivyo mavuno huongezeka.
Utayarishaji
wa mbegu.
Mbegu
iandaliwe mapema mwezi mmoja kabla ya kupanda na pia itunzwe katika mazingira
mazuri kwenye kivuli pasipo na jua ikiwezekana weka ndani ya chumba
kinachopitisha hewa, pindi unapokwenda kupanda katakata vipande urefu wa nchi
moja na hakikisha tunguu haijakauka. Kiasi cha kilo 840-1700 cha vipande vya tunguu
huweza kutumika kwa kupanda katika hekta moja.
Upandaji
Zao
la tangawizi hupandwa kwa kutumia vipande vya tunguu vyenye kichipukizi kizuri
angalau kimoja na huweza kukatwa katika urefu wa sm.2.5-5. Tangawizi humea na
kukomaa baada ya miezi 8 mpaka 10. Wakati mwingine, vichipukizi vinavyopatikana
katika kumenya tangawizi huweza kuhifadhiwa na kutumika kwa kupanda.
Kiasi
cha kilo 840-1700 cha vipande vya tunguu huweza kutumika kwa kupanda katika
hekta moja. Nafasi inayotumika kupanda ni kati ya sentimita. 23-30 kwa 15-23 na
kina cha sentimita.5-10 na mara nyingi hupandwa katika matuta. Baadhi ya mazao
huweza kupandwa katika shamba la tangawizi ili kuweka kivuli chepesi ingawa si
lazima kivuli kiwepo. Inashauriwa kumwagilia maji endapo mvua inakosekana. Na
inahitaji uangalizi kwa matokeo bora.
Mbolea
Weka mbolea za asili zilizooza vizuri kiasi cha ndoo moja hadi mbili, kwa eneo
la mita mraba 10. Mbolea hii iwekwe katika kila shimo. Kiasi kinachotakiwa ni
kilo moja au kopo moja la Tanbond kwa kila shimo. Hii ni sawa kuweka na tani 10
hadi 20 kwa hekta. Baada ya wiki 1-2 kabla ya kupanda weka mbolea ya samadi au
mboji kiasi cha tani 25-30 kwa hekta na kwa kukuzia weka kiasi cha NPK kwa uwiano wa kilo 36:36:80. Tandaza nyasi
shambani kuhifadhi unyevunyevu hasa pale kivuli kinapokosekana.
Upandaji.
Palizi hufanywa mara magugu yanapoota, dawa ya kuua magugu, kama simazine
hutumika. pandishia tuta ili kufanya tangawizi kutunza unyevu na huota vizuri
Magonjwa
na wadudu.
• Madoa ya majani yanayosababishwa na viini vya magonjwa viitwavyo Colletotrichum zingiberis na Phyllosticta zingiberi.
• Kuoza kwa tunguu; kunasababishwa
na viini viitwavyo Pithium spp • Mizizi fundo; inasababishwa na Meloidegyne
spp.
Uvunaji.
Tangawizi huweza kuwa tayari kwa kuvuna kati ya miezi 9-10 baada ya kupanda,
wakati majani yake yanapogeuka rangi kuwa njano na mashina kusinyaa. Tangawizi
inayohitajika kwa kuhifadhi kwenye kemikali (preserved ginger in brine) huvunwa
kabla haijakomaa kabisa, wakati ile iliyokomaa kabisa huwa kali zaidi na huwa
na nyuzi hivyo hufaa kwa kukausha na kusaga. Mavuno hutofautiana kulinganana na
huduma ya zao, mavuno yanaweza kuwa kiasi cha tani 20-30 cha tangawizi mbichi
huweza kupatikana.
Usindikaji.
Tangawizi ikisindikwa utapata unga, mafuta maalum (essential oils) n.k.
Tangawizi iliyovunwa huweza kumenywa, kukatwa na kukaushwa juani au mara
nyingine huchovywa katika maji yaliyochemka kwanza na ndipo kukaushwa au
hukamuliwa mafuta. Pia tangawizi husindikwa na kuhifadhiwa kwenye chupa zikiwa
zimechanganywa na sukari na/au chumvi. Hata hivyo tangawizi ina Kiasi cha
mafuta cha 16.0-18.0%.
Subscribe by Email
Follow Updates Articles from This Blog via Email

No Comments