Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais, Menejimenti ya Utumishi wa Umma na
Utawala Bora, Angellah Kairuki amesema tayari serikali imetoa kibali cha
ajira 15,000 kwa ajili ya kujaza nafasi zilizoachwa wazi na watumishi
waliofutwa kazi baada ya waliobainika kuwa na vyeti vya kughushi katika
kada mbalimbali.
Waziri Kairuki ameyasema hayo leo bungeni alipokuwa akijibu swali la
Mbunge wa Viti Maalumu Mkoa wa Iringa, Ritta Kabati aliyetaka kujua
mpango wa serikali kuhusu kujaza nafasi zilizoachwa wazi na watumishi wa
umma walioacha kazi kufuatia agizo la Rais Magufuli alilolitoa mapema
Mei mwaka huu.
Waziri Kairuki alisema kuwa ni kweli baada ya watumishi hao kuondoka
katika vituo vyao vya kazi, sehemu mbalimbali zilikumbwa na uhaba wa
watumishi na hivyo kupelekea kuzorota kwa utoaji wa huduma. Lakini ili
kukabailiana na hilo, hivi karibuni serikali imetoa kibali cha kuajiri
watumishi wapya kujaza nafasi hizo.
Mei mwanzoni Rais Magufuli aliagiza hadi Mei 15 mwaka huu watumishi wote
waliotajwa katika orodha ya wenye vyeti vya kughushi waondoke mara moja
la si hivyo watachukuliwa hatua za kisheria.
Subscribe by Email
Follow Updates Articles from This Blog via Email

No Comments