Muigiza wa Filamu nchini, Riyana Ally na mumewe ambaye ni msanii wa
Bongo Fleva, Leo Mysterio wamesema hawaoni aibu kuishi pamoja kisa umri.
Wakizungumza katika kipindi cha Twenzetu cha Times FM, Riyama amesema
yeye binafsi haoni aibu wala hana hofu kuolewa na mwanaume ambaye yeye
amemzidi umri zaidi ya miaka saba. Kwa upande wake Leo Mysterio ameeleza
wakati anataka kumuoa Riyama alisemwa sana na kukosolewa vikali.
“Eti kwa sababu umri ni mkubwa lakini kwa sababu sisi ni watu wa dini
haikua kazi kumaliza swala la ndoa. Niliwahi kutoa wimbo maalum kwa
ajili ya Riyama na ilinitoka moyoni kabisa kitu ambacho kiliwashangaza
wengi,” amesema Leo Mysterio
Subscribe by Email
Follow Updates Articles from This Blog via Email

No Comments