Diva wa Bongo Movie Jacqueline Wolper amesema kuwa haoni haja ya kuwa
na mahusiano kwa wakati huu, japo kuwa wanaume wengi wenye pesa wamekuwa
wakimsumbua kumtaka kimapenzi, na kwamba anaamini ni wasumbufu tu na
hawana mapenzi ya kweli.
Wolper amefunguka hayo karibuni na kusema kwama kutokana na upendo wa
kweli anaojitahidi kumuonyesha mwanaume anapokuwanaye kwenye uhusiano
na kujikuta akiambulia maumivu, ameona bora aweke kando masuala ya
mapenzi na kuwa`bize’ na kazi zake.
“Sina mpenzi kwa sasa nimeona bora niweke pembeni haya mambo nidili
na kazi zangu tu ndo muhimu, nikisema nipende hawa wanaonisumbua `now’
nitapenda sana na nitakuwa kimapenzi, lakini bado wote wanaonisumbua
hakuna aliyefaulu kunishawishi niwe naye,” alisema Wolper.
Wolper kwa sasa amekanusha kuwepo kwenye mahusiano baada ya kuachana na mpenzi wake ambaye ni mwanamuziki hivi karibuni
Subscribe by Email
Follow Updates Articles from This Blog via Email

No Comments