Monday, July 17, 2017

thumbnail

Hivi Ndivyo Watu Wawili Walivyokufa Wakati Wakibatizwa


Watu wawili wanaripotiwa kufariki wakati wakibatizwa siku ya Jumapili, kwenye mto ulio eneo la Rombo mkoa wa Kilimanjaro Kaskazini mwa Tanzania.

Kwa mujibu wa naibu kamanda wa polisi Hamisi Selemani Issa, watu hao walikuwa wakibatizwa kwa kuzamishwa ndani ya maji, katika zoezi lililokuwa likiendeshwa na mhubiri wa Kanisa la Shalom huko Rombo.

Walizama maji katika mto Ungwasi wakati walikuwa wakizamishwa baada ya kile kinachotajwa kwa kulemewa na mawimbi makali ya mto huo.

Haijulikani ni kwa njia gani mhubiri na waumini wengine waliokuwa wakiendesha zoezi hilo walinusurika.

Polisi baadaye waliitwa kuondoa maiti baada ya ajali hiyo.

Naibu kamanda wa polisi aliiambia BBC kuwa waumini wa kanisa akiwemo pia mhubiri wamezuiliwa ili kuhojiwa.

Subscribe by Email

Follow Updates Articles from This Blog via Email

No Comments

About

Powered by Blogger.

Facebook

STORI ZA NYUMA

DESIGNED BY: SEETHEAFRICANLINK

MICHEZO

3/SPORTS/small-col-left

HABARI

3/GENERAL NEWS/small-col-left

UDAKU

3/GOSSIP/small-col-left

BURUDANI

3/ENTERTAINMENT/small-col-left

Fashion

Nature

Business

Main Slider

10/slider-recent

Music