Monday, July 3, 2017

thumbnail

Samsung kuingiza simu mpya sokoni baada ya kufeli kwa Galaxy Note 7

Muonekano wa simu mpya za alaxy Note Fan Edition

Baada ya Samsung kulazimika kusitisha utengenezaji wa simu za Galaxy Note 7 kutokana na tatizo lake la kulipuka, kampuni hiyo imeamua kuja na simu mpya ya Galaxy Note Fan Edition.

Kwa mujibu wa taarifa iliyotolewa na kampuni hiyo imedai, utengenezwaji wa simu hizo umetokana na baadhi ya vitu kutoka katika simu ya Galaxy Note 7 ambayo ilisitishwa kuingia sokoni tangu mwezi septemba mwaka jana kutokana na kuleta madhara kwa baadhi ya watumiaji kutokana na mlipuko kwenye simu hizo.
Taarifa imeendelea kwa kusema simu hizo mpya zitaanza kuuzwa Julai 7 mwaka huu nchini Korea Kusini ambapo ndipo yalipo makao makuu ya kampuni hiyo.

Simu za Galaxy Note 7 zilikadiriwa kuuza kiasi cha dola bilioni 5.3 duniani kote ikiwa ni muda mfupi tangu ziingie sokoni lakini baada ya kusitishwa kwa uuzwaji wake inadaiwa kampuni hiyo ilipata hasara ya takribani dola bilioni 10.
Picha ya simu za Galaxy Note 7 ambazo zilisitishwa kutengenezwa kutokana na kulipuka

Subscribe by Email

Follow Updates Articles from This Blog via Email

No Comments

About

Powered by Blogger.

Facebook

STORI ZA NYUMA

DESIGNED BY: SEETHEAFRICANLINK

MICHEZO

3/SPORTS/small-col-left

HABARI

3/GENERAL NEWS/small-col-left

UDAKU

3/GOSSIP/small-col-left

BURUDANI

3/ENTERTAINMENT/small-col-left

Fashion

Nature

Business

Main Slider

10/slider-recent

Music