Naibu Waziri wa Mambo ya Ndani ya Nchi, Mhe. Hamad Masauni amesema kuwa Suala la kumaliza uhalifu kibiti na mkulanga ni suala ambalo halina mjadala ni suala la lazima.
Hayo yamezungumzwa jana na Naibu Waziri wa Mambo ya Ndani, Hamad Masauni wakiongea na waandishi wa habari kuhusu mauaji yanayoendelea maeneo ya Kibiti, Rufiji na Mkuranga.
“Suala la kumaliza uhalifu Kibiti na Mkuranga ni suala ambalo halina mjadala, ni suala la lazima lakini suala ni lini uharaka wake ndio maana leo tumejadili changamoto zinazokabili ili tuweze kukaa kwa pamoja tuweze kuzifanyia kazi. Ili tuweza kuharakisha zoezi hili ambalo kwa hakika kwa uwezo wa Mwenyezi Mungu kwa sisi tunaosimamia haki na uhai wa raia wasio kuwa na hatia hii vita lazima tushinde inshaallah,” alisema Masauni.
Subscribe by Email
Follow Updates Articles from This Blog via Email

No Comments