Msanii wa muziki wa dansi, Chaz Baba.
Msanii wa muziki wa dansi nchini Tanzania, Chaz Baba amefunguka kwa kudai muziki wa dansi hawezi kufa kama wasanii wake wangali wapo hai huku akisisitiza kwamba na kama ukifa basi heshima ya 'Live band' itaendelea kuwepo.
"Wengi wanasema muziki wa dansi umekufa lakini nasema kuwa hakuna wakuua muziki wa dansi ikiwa wanamuziki wenyewe bado wapo hawajakufa, pengine labda wanamuziki wote wa dansi wakifa ndiyo utakapokufa muziki wenyewe", amesema Chaz Baba
Pamoja na hayo, Chaz Baba aliendelea kwa kusema "isitoshe pia, utaoa muziki wa dansi lakini heshima ya muziki wa 'Live' ubaki hata kwa wenzetu walioendelea 'play back' hakuna muziki ni 'Live' tu kwa hiyo ndiyo maana sisi waasisi tupo na wazima wa afya", amesisitiza Chaz.
Kwa upande mwingine, Chaz Baba amewataka wasanii wenzake waendeleze umoja wao waliyokuwa nao kipindi cha nyuma katika kushirikiana kazi zao za sanaa pamoja na kujitokeza endapo wamepata mualiko wa kufanya mahojiano na vyombo vya habari.
Mtazame hapa anavyofunguka mengine zaidi.
Subscribe by Email
Follow Updates Articles from This Blog via Email
No Comments