Friday, July 21, 2017

thumbnail

Umesikia kauli ya Chaz Baba?

Msanii wa muziki wa dansi, Chaz Baba.

Msanii wa muziki wa dansi nchini Tanzania, Chaz Baba amefunguka kwa kudai muziki wa dansi hawezi kufa kama wasanii wake wangali wapo hai huku akisisitiza kwamba na kama ukifa basi heshima ya 'Live band' itaendelea kuwepo.

Chaz Baba amebainisha hayo kupitia kipindi cha eNewz kutoa EATV baada ya kuwepo imani ya kwamba muziki wa dansi umekufa  nchini Tanzania kutokana na kutosikika kwa muda mrefu wasanii wake wakiwa wanatumuiza katika majukwaa ya burudani.

"Wengi wanasema muziki wa dansi umekufa lakini nasema kuwa hakuna wakuua muziki wa dansi ikiwa wanamuziki wenyewe bado wapo hawajakufa, pengine labda wanamuziki wote wa dansi wakifa ndiyo utakapokufa muziki wenyewe", amesema Chaz Baba

Pamoja na hayo, Chaz Baba aliendelea kwa kusema "isitoshe pia, utaoa muziki wa dansi lakini heshima ya muziki wa 'Live' ubaki hata kwa wenzetu walioendelea 'play back' hakuna muziki ni 'Live' tu kwa hiyo ndiyo maana sisi waasisi tupo na wazima wa afya", amesisitiza Chaz.

Kwa upande mwingine, Chaz Baba amewataka wasanii wenzake waendeleze umoja wao waliyokuwa nao kipindi cha nyuma katika kushirikiana kazi zao za sanaa pamoja na kujitokeza endapo wamepata mualiko wa kufanya mahojiano na vyombo vya habari.
Mtazame hapa anavyofunguka mengine zaidi.

Subscribe by Email

Follow Updates Articles from This Blog via Email

No Comments

About

Powered by Blogger.

Facebook

STORI ZA NYUMA

DESIGNED BY: SEETHEAFRICANLINK

MICHEZO

3/SPORTS/small-col-left

HABARI

3/GENERAL NEWS/small-col-left

UDAKU

3/GOSSIP/small-col-left

BURUDANI

3/ENTERTAINMENT/small-col-left

Fashion

Nature

Business

Main Slider

10/slider-recent

Music