Msanii wa Bongo Flava, Vanessa Mdee ameeleza sehemu ya pili ya maisha yake katika michezo kwa kusema yeye ni shabiki mkubwa wa Manchester United.
Muimbaji huyo ambaye kwa sasa anafanya vizuri na ngoma yake mpya ‘Kisela’, amekiambia kipindi cha Leo Tena cha Clouds Fm kuwa tangu high school alikuwa mpenzi wa mpira wa miguu na ndio sababu ya kuwa shabiki wa Man United pia kuna wachezaji wanamvutia zaidi katika klab hiyo.
“Ndiyo kuna wanaonivutia, nampenda sana mchezaji mmoja anaitwa Patrice Evra hasa sasa hivi namfuatlia kwenye mitandao ya kijamii zamani alikuwa anaichezea Man United sasa hivi amehama anachezea timu flani hivi, page yake ya instagram ni ya kuvutia na kuhamasha vijana, very positive, so his my favorite right now, lakini zaidi nampenda Zalatan Ibramovich,” amesema Vanessa.
Subscribe by Email
Follow Updates Articles from This Blog via Email

No Comments