Monday, July 10, 2017

thumbnail

Yusuf Mlela afungukia kifo chake


MWIGIZAJI wa Bongo Muvi, Yusuf Mlela amesimulia mazingira yote ya namna alivyonusa kifo, kufuatia ajali aliyoipata hivi karibuni iliyosababisha kulazwa hospitalini kwa siku kadhaa.

Mlela aliliambia Wikienda kuwa, alipata ajali hiyo ya gari huko Mombasa nchini Kenya, majira ya usiku alipokuwa akielekea klabu kuhudhuria shoo ya wasanii kutoka Bongo, Ben Pol na G-Nako, baada ya gari alilokuwa akitumia na rafiki zake kupoteza mwelekeo na kugonga kalavati na kuviringika mara mbili, hivyo akapoteza fahamu na kuchanika sehemu ya juu ya mdomo ambapo alipozinduka akajikuta hospitalini.

Mlela alisema kuwa, waliondoka nyumbani kwa mwendo wa kawaida, lakini wakiwa njiani gari lilianza kuyumba na baadaye dereva kushindwa kulidhibiti hivyo kuparamia ukingo wa kalavati hilo.

“Ninamshukuru sana Mungu kwa kuninusuru na roho ya kifo vinginevyo sasa stori ingekuwa tofauti kabisa, ajali isikie kwa wengine, nashangaa hata huu mdomo umeponaje na kurudia hali yake ya kawaida maana ulichanika ile mbaya,” alisema Mlela.

Subscribe by Email

Follow Updates Articles from This Blog via Email

No Comments

About

Powered by Blogger.

Facebook

STORI ZA NYUMA

DESIGNED BY: SEETHEAFRICANLINK

MICHEZO

3/SPORTS/small-col-left

HABARI

3/GENERAL NEWS/small-col-left

UDAKU

3/GOSSIP/small-col-left

BURUDANI

3/ENTERTAINMENT/small-col-left

Fashion

Nature

Business

Main Slider

10/slider-recent

Music