Monday, July 3, 2017

thumbnail

Nikikutana na Rais Magufuli natangaza matatizo yangu – Roma Mkatoliki


Msanii wa muziki wa hip hop, Roma Mkatoliki ameweka wazi akipata nafasi ya kukutana ana kwa ana na Rais John Pombe Magufuli, atakachofanya ni kumweleza tu shida zake binafsi ili asaidiwe kutimiza ndoto zake.
Rapa huyo amedai unapokutana na Rais kwa dakika chache ni fursa kubwa hivyo lazima uitumie vizuri kwani ukisema uanze kueleza matatizo ya wananchi unaweza kukosa nafasi ya kueleza mambo yako kutokana na kukosa muda.
“Nikikutana na Rais nitamweleza matatizo yangu, anisaidie matreka na mahitaji yangu mengi binafsi. Ukikutana na Rais hutakiwi kupoteza muda kuanza kumwelezea shida za wananchi, nampiga kizinga tu Mh hapa nilipo sina kitu kabisa,” Roma alikiambia kipindi cha Enewz cha EATV.
Aliongeza,”Mimi wakati nafanya wimbo wa Mr President mwaka 2011 nilieleza ndani ya ule wimbo nikikutana na Rais nitamweleza nini, mule nimeyaeleza mambo mengi sana na nilitumia kama dakika tano kueleza yote hayo. Changamoto kubwa ukikutana na waheshimiwa unapata muda mchache sana wa kuzungumza nao, dakika moja, mbili au tatu na hizo dakika huwezi kumwambia kero za wananchi, dakika tatu unamwambia Mh mimi naomba unisaidie hiki na hiki niendeshe familia yangu,”
Rapa huyo hivi karibuni alifanya show yake ya kwanza katika ukumbi wa Dar Live ikiwa na mwezi mmoja na nusu toka atekwe na watu wasiojulikana na baadaye kuachiwa.

Subscribe by Email

Follow Updates Articles from This Blog via Email

No Comments

About

Powered by Blogger.

Facebook

STORI ZA NYUMA

DESIGNED BY: SEETHEAFRICANLINK

MICHEZO

3/SPORTS/small-col-left

HABARI

3/GENERAL NEWS/small-col-left

UDAKU

3/GOSSIP/small-col-left

BURUDANI

3/ENTERTAINMENT/small-col-left

Fashion

Nature

Business

Main Slider

10/slider-recent

Music